Israeli imeendelea kuivirumishia makombora Gaza kucha kutwa
,huku kikao cha mawaziri wa baraza la Usalama kikitarajiwa huko Marekani
kujadili mapendekezo mapya ya wito wa kusitishwa mapigano kwa misingi ya
kibinadamu.
Idadi ya raia wa Palestina waliouawa imezidi mia nane, huku mashambulio hayo ya Israel ya angani majini na ardhini yakiingia siku ya kumi na nane.
Wanajeshi 32 na raia watatu wa Israel wameuawa katika muda huo.Katika ukingo wa magharibi, na Jerusalem mashariki raia wawili wa Palestina wameuawa na wengine wengi kujeruhiwa wakati waandamanaji waliokuwa na hasira kuhusu mashambulio huko Gaza walipokabiliana na vikosi vya Israel.
No comments:
Post a Comment